Kuna mambo mengi sana ambayo ni muhimu kuyajua katika maisha na kujua aina mbalimbali za watu, kujifunza namna ya kuwasoma wanadamu, na kujua namna ya kutofautisha kati ya kuwa na watu wanaotufaa na wasio tufaa. Ni bora na muhimu sana kujiweka karibu na watu wa aina zote na kujua huyu ana akili gani na huyu ni wa aina gani kwa kuangalia utu wao, tabia zao, mwenendo wao, matendo yao na jinsi wanavyoweza kupambanua mambo. Ni muhimu kujua hili, baadhi ya watu huja katika maisha yako kama Baraka kwa kuwa wanakufaa sana katika maisha na wa kweli kwa kwako, kamwe hawawezi kukudanganya na kamwe hawawezi kukusaliti ama kukuondolea imani nao, hawa siku zote ni kama uti wa mgongo wako , ni sehemu ya maisha yako na huishi nawe bila ya kutafutiana au kuwekeana madoa.

Lakini kuna baadhi ya watu huja katika maisha yako kutoa somo tu, wakati mwingine urafiki, mahusiano vinaenda tofauti na vile ulivyo tarajia ama kukusudia katika maisha yako kutokana na kundi hili la watu na hapo ndipo swala la kujifunza linakuja. Kwani utaona rangi halisi ya mtu , utu halisi wa mtu, mwenendo halisi wa mtu na tabia yake halisi hujitokeza muda huu. Hatua hii ndipo utawajua watu na baadhi ya watu wana karama (gift) kuwasoma wenzao papo kwa papo na kujua huyu ni mtu wa aina gani kwa kuangalia tu baadhi ya mambo kama vile, macho, jinsi anavyoonesha sura yake na matendo halisi ya mwili wake kama vile kujitikisa, geuka geuka n.k hapa waswahili wanaita –body language.

Vitendo vya mtu na macho yake vinaonesha sana kuwa huyu ni mtu wa namna gani? Naona unajiuliza Boniface anaongea nini hapa… nasema hivi, kuna watu wana uwezo wa kumtazama mtu maramoja na wakaeleza mambo ambayo mtu mwingine kamwe hawezi kuyaona hata iweje. Sote tunatakiwa kujifunza namna ya kuwasoma watu na kuwa wahukumu wazuri wa tabia za watu. Ukijifunza hili litakusaidia sana katika maisha yako ya kila siku na yajayo katika kutengeneza marafiki, mahusiano na mambo mbalimbali yanayohusiana na kushirikiana. Ni muhimu sana kuwa makini kabla ya kumwamini mtu na kumpa moyo wako wote, ufahamu wako wate na roho yako pia. Ni rahisi sana kudanganywa na watu ambao wao wanauwezo mkubwa wa kudanganya kwa mambo ambayo tunatamani kuyasikia na wanajaribu sana kukonga nyoyo zetu kwa kubadili akili zetu na mitazamo yetu, kumbuka hutumia mbinu za ziada au triki kali sana. Kujifunza mambo ya muhimu katika maisha ni jambo la muhimu sana, itatusaidia kukua, itatusaidia kwa matatizo yasiyoisaha yanayoweza kujitokeza muda wowote, na hata mambo mapya katika maisha ambayo yulikuwa bado hatujayakabili au kuyafikia. Kuna aina zote za watu katika dunia hii; kuna tabia nyingi sana na mambo mengi kutokana na mazingira halisi. Kwa kadri unavyojinza zaidi ndivyo tunavyozidi kuwa na uwezo zaidi wa kukabiliana na watu, kukabiliana na hatua mbalimbali za ukuaji wa mtu katika maisha yetu. Tunatakiwa kujifunza kutokuamini haraka na kujifunza kutokutoa kwa asilimia mia moja vinginevyo utoapo asilimia mia moja zako uwe na uhakika na kile ukifanyacho. Wakati mwingine maisha yanaweza kuyeyusha kitu kigumu, lakini tunahitaji kuwa imara na tunahitaji kufunga kurasa mbaya tulizopitia na kufungua kurasa safi kwa umakini.

Ndugu zangu, Maisha matamu sana lakini mafupi mno. Kila jambo hutokea kwa sababu fulani, iwe nzuri ama mbaya lakini ni sababu murua, kuna watu wanakuja katika maisha yako na wengine wanatoka kutoka na sababu mbalimbali. Sote tupo katika njia tofauti katika maisha na muhimu zaidi ni nani tunamchukua kuwa nasi katika hii safari na nani tunashirikiana naye naye au nao pamoja. Kuwa na furaha, kuwa na mtazamo chanya, jasiri, mhalisia wa maisha. Kama mambo ni magumu, yanayumba na yanakusononesha kwako sasa, siku zote kumbuka kuwa hakuna masika yasiyo kuwa na ncha. Mungu yupo siku zote kutulinda na kututazama kwa msaada. Kujifunza masomo muhimu tunayopitia katika maisha ni jambo ambalo litakusaidia sana katika maisha ya usoni au mbeleni. Japokuwa mara nyingi hawaamini kama ipo siku wakao-nyookewa kwa matumaini kidogo, mambo makubwa huja kwa uvumilivu, ustahimilivu na maono ya kimikakati. Tunapotegemea na kuendelea kutegemea, ianaweza kuchukua muda nab ado matokeo yakawa tofauti na matarajio yetu. Usikae unatafakari mategemeo yako muda wote, wewe fanya kazi, soma, n.k usijitie nuksi (don’t jinx yourself) usijikandamize mwenyewe na mawazo. Acha watu wazuri katika maisha yako waje kwa nguvu ya asilia au naturall. Hakika Mungu atakuweka katikati ya kundi la watu wema na kila kitu kitakuwa sawia kwako.

Najua fika muda mwingine mambo hayaleti maana kabisa kwa namna gani maisha yako yalivyo au watu ulionao karibu. Tunahitaji kuwa watu wa mtazamo wa mbali na kujikita katika kufanya kazi au kusoma alama za nyakati. Fanya lisilowezekana, liwezekane bila majuto, hakuna kurudi nyumana fanya kile ambacho ni bora kwako wewe ili kupata raha yako mwenyewe na ndoto zako na matakwa yako yatimie. Lazima itokee yatimie, penye nia pana njia siku zote na kwa kila jambo. Anza kujaribu, kwa muda mfupi utaona mabadiliko. Usiogope, kuwa na furaha na endelea kusongesha gurudumu lako la maisha.

Kama somo hili linaeleweka basi nitie moyo kwa kusema asante ukisoma na kama halieleweki uliza ntafafanua nikitulia..


   Mwandishi wa makala hii anapatikana pia:

fb Facebook        twitt  Twitter           link LinkedIn


8 thoughts on “BAADHI YA WATU HUJA KATIKA MAISHA YAKO KAMA BARAKA, BAADHI KAMA MASOMO TU.

  1. Hello! I know this is kinda off topic but I was wondering which blog
    platform are you using for this site? I’m getting
    fed up of WordPress because I’ve had issues with hackers and I’m looking at alternatives for
    another platform. I would be fantastic if you could point me in the direction of a good platform.

  2. She stepped forward and placed her first two fingers in the deepest
    part she could see and it felt luke warm and silky to the
    touch as nauseatingly as she suspected. Palm hand side up: Pull hand up
    so fingers point towards the sky. Spalding Official NBA Varsity Junior Outdoor Basketball
    for $8.

  3. I usually do not drop many comments, but after browsing
    through a few of the remarks on BAADHI YA WATU HUJA KATIKA MAISHA YAKO KAMA
    BARAKA, BAADHI KAMA MASOMO TU. | Boniface Evarist Blog.
    I actually do have 2 questions for you if you tend not to mind.
    Could it be only me or do some of these comments appear
    like they are left by brain dead folks? 😛 And, if you are writing at
    other sites, I would like to follow you. Would you post a list
    of the complete urls of your social community pages like your twitter feed, Facebook page or linkedin profile?

  4. Hi there, I discovered your blog by the use of Google even as looking for a related subject, your
    website came up, it seems great. I’ve bookmarked it in my google bookmarks.
    Hi there, simply become alert to your blog through Google, and found that it is really informative. I’m going
    to be careful for brussels. I will be grateful when you proceed this in future.

    Numerous folks shall be benefited from your writing.
    Cheers!

  5. You’re so interesting! I don’t think I’ve truly read something like this before. So nice to find someone with original thoughts on this topic. Seriously.. many thanks for starting this up. This website is something that is needed on the internet, someone with a bit of originality!

Leave a reply to referencement de site Cancel reply